Daima Mimi Mkenya Lyrics – Eric Wainaina

Song Info: Daima Mimi Mkenya Song name is Daima sung by Eric Wainaina.

Daima Mimi Mkenya Lyrics

[Mstari 1]

Umoja ni fahari yetu
Undugu ndio nguvu
Chuki na ukabila
Hatutaki hata kamwe
Lazima tuungane, tuijenge nchi yetu
Pasiwe hata mmoja
Anaetenganisha

[Chorus]
Naishi, Natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu
Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

[Mstari 2]

Kwa uchungu na mateso
Kwa vilio na uzuni
Tulinyakuliwa Uhuru
Na mashujaa wa zamani
Hawakushtushwa na risasi
Au kufungwa gerezani
Nia yao ukombozi kuvunja pingu za ukoloni

[Chorus]

Naishi, Natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu
Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo
[Daraja]

Wajibu wetu
Ni Kuishi kwa upendo
Kutoka ziwa Mpaka pwani
Kaskazini na kusini

[Solo]

[Chorus]

Naishi, Natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu
Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

[Mwisho]

Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Music Video

Leave a Comment